728x90 AdSpace

Latest News

WATANASHATI CLASSICS. Powered by Blogger.
Monday 18 July 2016

BASATA HAWAJANIPA MAJIBU KAMILI;ROMA



Msanii wa Hip Hop Bongo, Roma amesema kuwa Baraza la Sanaa la Taifa, Basata limeshindwa kumpatia majibu ya msingi juu ya sababu ya kufungiwa kwa nyimbo yake ya ‘Viva Roma Viva’.

Msanii huyo amekiambia kipindi cha ‘Hatua Tatu’ cha Times FM kuwa Basata wameshindwa kumpa sababu za msingi juu ya kufungia wimbo wake.
“Siwasemei wengine lakini mimi nilijaribu kuwauliza Basata kwanini wamefungia wimbo wangu lakini sikupewa majibu ya msingi na yenye kueleweka,” alisema Roma.
Basata waliufungia wimbo wa Roma ‘Viva Roma Viva’ mwezi October mwaka jana kwa madai kuwa wimbo huo umekiuka maadili kutokana na kuchochea ugomvi.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: BASATA HAWAJANIPA MAJIBU KAMILI;ROMA Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top